Mukhisa Kituyi wa Kenya (kuzaliwa 1956) alikuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa juu ya Biashara na Maendeleo, UNCTAD kutoka mwaka 2013 hadi 2021. Hapo awali alikuwa Afisa Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya Utawala Bora, Kenya, mjini Nairobi. Aliwahi pia kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara kuanzia mwaka 2002 hadi 2007.